• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

DC AAGIZA KUSOMWA KWA MAPATO NA MATUMIZI

Posted on: March 23rd, 2017



Viongozi wa Vijiji vyote Wilayani Ikungi Mkoani Singida wameagizwa kusoma mapato na matumizi ili kuwarahisishia wananchi kufahu jinsi fedha zao zinavyotumika katika ukweli na uwazi na kutoa fursa kwa wananchi kupata nafasi ya kuhoji ili kujiridhisha pale wanapokuwa na mashaka.


Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu wakati wa mikutano yake ya kazi katika Wilaya hiyo iliyoanza jana kwa kutembelea kila kata kukagua miradi ya maendeleo na kufanya mikutano ya hadhara yenye lengo la kujua maeneo ya utendaji na kuwakumbusha wenyeviti na watendaji wa Vijiji na Kata kutambua majukumu yao na kuyapatia majibu sawia na kubadili changamoto kuwa fursa.


Dc Mtaturu ameagiza kufanyanyika uchunguzi ili kubaini kama kuna watendaji wamehamishwa kazi na wanatuhumiwa kuhujumu mapato ya serikali na michango ya wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo kurudishwa haraka iwezekanavyo ili kutoa majibu ya tuhuma hizo na kuchukuliwa hatua endapo watabainika kujihusisha na kadhia hiyo.


Katika mkutano uliofanyika katika Kata ya Ntuntu na Kata ya Lighwa Dc Mtaturu amesema kuwa wazazi wote ambao watoto wao wanajihusisha na utoro watachukuliwa hatua haraka iwezekanavyo ili kubaini chanzo cha utoro huo kama unasababishwa na wazazi wenyewe ama wanafunzi kujihusisha na makundi ovu ikiwemo kufanywa vijakazi katika maeneo ya mijini.


Dc Mtaturu amewakemea wanasiasa ambao wamezuia wananchi kuchangia ujenzi wa nyumba za walimu, Ujenzi wa Shule na maabara huku wakiwaahidi kuwa serikali itajenga kila kitu na kuongeza kuwa serikali kuu haiwezi kufanya kila jambo badala yake wananchi kwa umoja wao wanapaswa kushiriki katika uchangiaji wa huduma za kijamii.


Mkuu huyo wa Wilaya amewaagiza watumishi wote wa serikali ngazi ya Vitongoji, Vijiji na Kata kufanya kazi kwa haki, Usawa na uwazi na kiwashirikisha wananchi katika kila jambo linalohusu vipaombele vya maeneo yao.


Pia amevitaka vijiji 39 ambavyo havijapimwa kupimwa na kurahisisha upangaji wa matumizi bora ya ardhi ili kuepuka migogoro mbalimbali ya ardhi ambayo imekuwa ni changamoto kubwa katika maeneo mengi nchini.


Akizungumzia kadhia ya maji safi na salama kati kata hizo mbili Dc Mtaturu alisema kuwa serikali inatambua kuwa hakuna maji safi na salama hivyo imejipanga kuzikabili changamoto hizo katika kipindi cha muda mfupi.


Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo wamempongeza mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kufanya ziara katika Kata hizo kwani wana miaka zaidi ya 10 hawajawahi kutembelewa na Mkuu wa Wilaya wala Mkurugenzi.


Wananchi hao wametoa mifano ya Wakuu wa Wilaya waliowahi kufika wakati huo Wilaya ikiwa haijagawanywa kitoka Wilaya ya Singida kuwa ni pamoja na aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Hawa Ngurume (Marehemu) sawia na Mhe Abas Kandoro ambaye hivi karibuni alistaafu akiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.


Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ameivunja kamati ya maji katika Kijiji cha Ntewa B iliyopewa mamlaka ya kuendeleza upatikanaji wa huduma ya maji na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Rustika Turuka kufatilia ili kujua chanzo cha kukosekana kwa maji katika kijiji hicho ilihali miundombinu ya kupatikana maji kijijini hapo imekamilika vyema.


Dc Mtaturu alisema kuwa Demokrasia inayohubiriwa na baadhi ya wanasiasa nchini inapaswa kuwa Demokrasia ya kweli kwa kuwa na nidhamu na mamlaka pia kutoitukana serikali na kupinga kila jambo linalofanywa na serikali.


Sambamba na hayo pia Dc Mtaturu amemuagiza Mkuu wa Polisi Wiliya ya Ikungi kuwakamata haraka iwezekanavyo wazazi wa watoto watatu ambao ni wanafunzi wa katika Shule ya Sekondari Lighwa waliopatiwa mimba ili kutoa taarifa ya watu waliowapa ujauzito huo na kuchukuliwa hatua.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa