• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Ikungi: Miradi ya Afya, Kilimo na Huduma za Jamii Yazingatiwa kwa Ukamilifu

Posted on: January 30th, 2026

Leo tarehe 30 Januari, 2026, Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi limeendelea na siku ya pili ya kikao chake kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri.

Akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mheshimiwa Ally Juma Mwanga, amewakumbusha Madiwani kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo, hususan wao kama wenyeviti wa kamati za maendeleo ya kata.

Amesisitiza umuhimu wa usimamizi wa karibu wa miradi hiyo ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Mwenyekiti Mwanga amebainisha zahanati zilizopo katika hatua za mwisho za ukamilishaji na kusisitiza zisimamiwe kwa karibu ili huduma za afya zianze kutolewa kwa wananchi. Zahanati hizo ni Unyampembe, Mtavira, Nkuninkana, Msule, Mduguuyu, Samaka na Makonda.

Amesema kuwa ni dhamira ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuona wananchi wanapata huduma bora, hivyo amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo, hususan ya sekta ya afya, zinatumika haraka na kwa ufanisi.

Wakati wa kufunga kikao hicho, Mwenyekiti Ally Mwanga aliwashukuru wajumbe wote wa Baraza kwa ushiriki wao mzuri na kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji kuongeza upatikanaji wa mbegu za mazao ya muda mfupi yanayotumia maji kidogo, ili kuwasaidia wakulima kukabiliana na changamoto ya upungufu wa mvua. Aidha, aliagiza matrekta yaliyotolewa na serikali yatumike mashambani kwa utaratibu uliowekwa, yakodishwe kwa bei nafuu kama ilivyoelekezwa, badala ya kubaki bila kutumika.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Bi. Haika Massawe, alimshukuru Mwenyekiti na Baraza la Madiwani kwa ushirikiano wao na kuahidi kuwa maelekezo yote yaliyotolewa yatafanyiwa kazi kwa haraka ili kuendelea kuimarisha maendeleo ya Halmashauri.

Katika kikao hicho, Baraza pia lilipokea na kujadili maazimio ya Kamati za Kudumu za Halmashauri, ambazo ni Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Kamati ya Kudhibiti UKIMWI, Kamati ya Huduma za Uchumi pamoja na Kamati ya Huduma za Jamii.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Dkt. Grace Ntogwisangu Awataka Watoa Huduma Zaidi Kutumia Teknolojia Kuboresha Chanjo

    February 04, 2026
  • Mhe. Thomas Apson Awapongeza Wadau Kwa Kuunga Mkono Shule ya Watoto Wenye Mahitaji Maalum

    February 03, 2026
  • Upandaji Miti na Msaada kwa Wagonjwa Vikundi Maalum Vifanyika Ikungi Kwa Ushirikiano na UWT

    February 03, 2026
  • imu ya Menejimenti ya CMT Yakagua Miradi ya Afya, Elimu na Biashara Ikungi

    February 02, 2026
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa