• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Ikungi Yapatiwa Trekta 15 Msimu wa Kilimo

Posted on: December 2nd, 2025

SERIKALI imetoa trekta ndogo 34 aina ya Power Tiller kwa halmashauri tano za Mkoa wa Singida ambazo zitakuwazinakodishwa kwa wakulima kwa bei nafuu waweze kuongeza uzalishaji ili ifikapo 2030 lengo la kilimo kuchagia asilimia 10 ya pato la taifa liweze kufikiwa.


Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Singida Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji, Stanslaus Choaji, akizungumza juzi wakati wa zoezi la kugawa ambalo lilifanywa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, alisema kuwa katika awamu ya kwanza Halmashauri za Wilaya ambazo zimepata mgao ni Halmashauri ya Wilaya Ikungi ambayo imepata Power Tiller 15, Mkalama 12, Singida DC 3, Iramba 2 na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imepata 2.


“Lengo la mpango huu wa serikali ni kufikisha zana za kilimo karibu na wakulima na kuwafanya wakulima waweze kupata huduma ya upatikaji wa zana za kilimo kwa bei nafuu ikilinganishwa na ile wanayokodi kwa watu binafsi hatimaye waweze kuongeza uzalishaji ili kufikia 2030 tuweze kufikia lengo la kilimo kuchangia asilimia 10 ya pato la taifa,” alisema.


Choaji alisema trekta hizo zitawekwa kwenye vituo vya zana za kilimo ngazi ya kata ambapo kutawekwa utaratibu wa namna ya kukodisha na kuwaomba wakulima kuhakikisha wanatumia zana hizo kuongeza maeneo ya kilimo ili waweze kulima kwa tija zaidi na kuongeza uzalishaji.


Alisema matarajio ya serikali ni kwamba baada ya wakulima kupata zana hizo uzalishaji utaongezeka maradufu ukilinganisha na ilivyo sasa kwasababu wakulima wataweza kuandaa mashamba mapewa kwa bei nafuu na pesa ambazo walikuwa wakizitumia kukodi matreka kwa watu binafsi sasa watazielekeza kununulia mbolea na mbegu za ruzuku.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida,Halima Dendego,akikabidhi ‘power tiller’ hizo kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, alisema baada ya kupata zana hizo jukumu liliobaki ni kuhakikisha kinazalishwa chakula cha kutosha pamoja na ziada kwa ajili ya kuuza ili kuongeza pato la kaya, mkoa na hatimaye pato la taifa.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Dkt. Grace Ntogwisangu Awataka Watoa Huduma Zaidi Kutumia Teknolojia Kuboresha Chanjo

    February 04, 2026
  • Mhe. Thomas Apson Awapongeza Wadau Kwa Kuunga Mkono Shule ya Watoto Wenye Mahitaji Maalum

    February 03, 2026
  • Upandaji Miti na Msaada kwa Wagonjwa Vikundi Maalum Vifanyika Ikungi Kwa Ushirikiano na UWT

    February 03, 2026
  • imu ya Menejimenti ya CMT Yakagua Miradi ya Afya, Elimu na Biashara Ikungi

    February 02, 2026
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa