Timu ya Menejimenti ya CMT ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Kastori Msigala, imefanya ziara leo tarehe 02 Februari 2026 kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kutoa maagizo ya kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa ubora.

Katika ziara hiyo, timu ilitembelea ujenzi wa vyumba 21 vya biashara Manispaa ya Singida vyenye thamani ya shilingi milioni 285, viwanja mbalimbali vya Halmashauri vinavyotarajiwa kuendelezwa mapema kadri bajeti itakavyotengwa lengo ni kutengeneza vyanzo vipya vya mapato kuleta maendeleo wilayani Ikungi

Katika hatua nyingine timu hiyo imetembelea nakagua maabara mbili katika Shule ya Sekondari Kintandaa zinazogharimu shilingi milioni 544.2, ambapo alisisitiza kukamilishwa haraka ili wanafunzi waanze kuzitumia.

Aidha, timu ilikagua Zahanati ya Ighombwe na kubaini matumizi mazuri ya mifumo ya GoTHOMIS na GePG, sambamba na kutoa maelekezo ya ukarabati wa zahanati hiyo na kukamilisha boma lililojengwa kwa nguvu za wananchi.
Katika Shule ya Sekondari Ighombwe, Mkurugenzi Mtendaji alikagua ujenzi wa maabara
ya Fizikia na Baiolojia unaogharimu shilingi milioni 60 pamoja na ukamilishaji wa bweni la wanafunzi lililojengwa kwa nguvu za wananchi.

Mwisho wa ziara, timu ilitembelea Zahanati ya Makhotea pamoja na ujenzi wa madarasa na vyoo Shule ya Msingi Makhotea unaogharimu shilingi milioni 123.2 kutoka BOOST na madarasa mawili ya shilingi milioni 46, ambapo miradi ipo hatua ya uezekaji.
Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania
Simu ya mezani: +255262964037/6
Mobile:
Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz
Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa