Leo tarehe 29.01.2025, Wilaya ya Ikungi imekuwa kitovu cha urithi wa taifa letu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa ushirikiano wa karibu na wadau wa maendeleo PELUM Tanzania, wameandaa na kufanikisha Maonesho ya Mbegu za Asili.

Maonesho haya yamepata hadhi ya kipekee kwa kuhudhuriwa na safu ya Waheshimiwa Madiwani, Watendaji wa Kata, pamoja na wakulima mahiri waliotoka maeneo mbalimbali ikiwemo Dodoma, Babati, Mwanga, Iramba, na wenyeji wao Ikungi.

Lengo kuu la maonesho haya limekuwa ni kuiamsha jamii na kuikumbusha juu ya umuhimu wa kutunza mbegu za asili. Kupitia ushirikiano huu, mkazo mkubwa umewekwa katika kuanzisha na kuimarisha Benki za Mbegu za Jamii (Community Seed Banks) zinazohakikisha mkulima anakuwa na mamlaka kamili juu ya kile anachopanda, bila kutegemea mbegu za kununua kila msimu.

Aidha, katika maonesho hayo, faida lukuki za mbegu hizi zimeelezwa kwa kina ikiwa ni pamoja na ustahimilivu wa ukame na mabadiliko ya tabianchi bila kutetereka.

Maonesho haya ya mbegu za asili yamekuwa ni daraja la kuunganisha mikoa na wilaya jirani katika harakati moja ya kuikomboa meza ya chakula ya Mtanzania na nimwanzo mpya wa safari ya kuelekea kwenye usalama wa chakula unaotokana na mbegu za asili
Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania
Simu ya mezani: +255262964037/6
Mobile:
Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz
Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa