• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Mradi wa "aware" kutokomeza matukio ya kikatili Ikungi

Posted on: August 17th, 2020

IOKOE NA UMASKINI yaani Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) ni Shirika lisilo la kiserikali ambalo siku hadi siku limekuwa likiakisi kwa vitendo malengo ya kuanzishwa kwake, ikiwemo utetezi wa haki na usawa wa kijinsia kwa wanawake, watoto na makundi mengine athirika.

Tangu kusajiliwa kwake takribani miaka sita iliyopita, SPRF imekuwa na kasi ya aina yake kwenye nyanja ya uwajibikaji, sanjari na ‘ari’ ya kujitoa na kuijali jamii, hususani kwenye maeneo ya kupunguza umaskini wa kipato na kutoa huduma za afya.

Shughuli nyingine za kikatiba zinazofanywa na shirika hilo ni pamoja na kujenga uwezo wa shirika endelevu na wadau wanaolizunguka ili kujiletea maendeleo.

Mkurugenzi Mtendaji wa SPRF nchini, Dkt Suleiman Muttani anasema kwa sasa shabaha iliyopo ni kuhakikisha wanaendeleza kasi ya kutekeleza mradi wa AWARE, baada ya kukamilika kwa kikao cha kimkakati cha kurasimisha mradi huo kwa mwaka 2020, kilichofanyika hivi karibuni.

“Kikao hicho tayari kimekwisha-fanyika na kilihusisha viongozi wa Wilaya ya Ikungi mkoani hapa, pamoja na watekelezaji wote wa sera na sheria, na kikubwa tuligusia masuala yaliyojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi kwa mwaka 2019, na tuliweka malengo na mwelekeo wa pamoja wa utekelezaji wake kwa mwaka 2020,” anasema Dkt Muttani.

Mkurugenzi huyo anasema kwa kipindi kirefu sasa, takribani miaka 4, SPRF chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS) imekuwa ikitekeleza mradi wa AWARE ndani ya Wilaya ya Ikungi unaofanya utetezi wa haki za wanawake na mtoto wa kike dhidi ya athari zitokanazo na mila na desturi zilizopitwa na wakati.

Muttani ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake nchini, anafafanua kwamba nguvu kubwa ya shirika hilo kwa sasa imeelekezwa zaidi kwenye Kata 2 za Siuyu na Dung’unyi kutokana na maeneo hayo kukithiri kwa matukio ya ukeketaji, mimba na ndoa katika umri mdogo, sanjari na ukatili dhidi ya wanawake na watoto na hasa mtoto wa kike.

Aidha, mara kadhaa aliishukuru serikali, FCS na wadau wengine kwa namna wanavyojali na kutambua juhudi mbalimbali zinazofanywa na SPRF katika mapambano ya kupinga na kufichua vitendo vya matukio ya ukatili wa kijinsia ndani ya jamii.

“Nakutaarifu Mkuu wangu wa Wilaya kuwa shirika letu limepata ruzuku ya milioni 30 kuendelea na utekelezaji wa mradi wa ‘AWARE’ kwenye Kata za Siuyu na Dung’unyi kutoka ‘the Foundation for Civil Society 2020,” anaeleza Muttani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo, kupitia hotuba yake iliyowasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Justice Kijazi, wakati wa kikao cha kurasimisha mradi wa AWARE kwa mwaka 2020, alisema anashukuru na kuupongeza uongozi wa SPRF nchini kwa kutekeleza mradi huo kwa ufanisi mkubwa.

“Mradi huu upo hapa Ikungi kwa miaka minne sasa…na sote tunashuhudia jinsi mradi huu unavyoendelea kuleta matokeo chanya katika vita dhidi ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni kwa vijana wetu walio katika umri mdogo, “ anasema Mpogolo.

Anasema mradi huo ulipiga hodi Ikungi mwaka 2017 na umeendelea kutekelezwa kwa mafanikio makubwa hadi kufikia Februari 2020. Na katika kipindi chote hicho walengwa wapatao 303, 944 walifikiwa.

Miongoni mwa idadi hiyo, walengwa wa moja kwa moja walikuwa 7932 huku wale wasio wa moja kwa moja idadi yao ikiwa ni 296,012.

“Kwa taarifa zilizopo walengwa wa moja kwa moja walifikiwa na SPRF wenyewe, na wale wasio wa moja kwa moja wakifikiwa na vikundi vya Sauti ya Mwanamke, Sauti ya Wanafunzi na Kamati za Ulinzi wa Mwanamke na Mtoto za vijiji (MTAKUWWA) chini ya uratibu wa SPRF,” anasema Mpogolo.

Mkuu huyo wa wilaya anasema njia zilizotumika kusambaza elimu na kuhamasisha ni pamoja na redio, magazeti, vipeperushi, majarida na mitandao ya kijamii.

Mpogolo Anaeleza kufurahishwa kwake na ushiriki wa Kamati za MTAKUWWA ngazi ya vijiji, Sauti za Wanawake za vijiji na zile za Wanafunzi hasa kutoka shule za Sekondari za Siuyu na Munkinya, Mungaa, Dadu, Puma na Miandi wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

Anasema vikundi hivyo vimekuwa chachu ya mabadiliko kwenye jamii zao, vikijikita katika kuhamasisha na kueneza elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia, ikiwa pamoja na kutembelea wenzao, kucheza ngoma zenye ujumbe na maudhui maalum, maigizo, mashairi, ngonjera na kufanya malumbano ya hoja.

“Kwenye eneo hili kauli yao ilikuwa ni ‘Simama Sema kwa Sauti Usikike:’ Ukimkata Hatulii,” anasema Mpogolo kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Ikungi, Kijazi.

Anatoa wito kwa jamii na wadau kuendelea kushikamana na kushiriki kikamilifu katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia katika sura zote…

“Hapa SPRF wametukumbusha wajibu wetu, na wametupa kazi ya kufanya, basi; na tuifanye kazi hii, na tuwe sote, tushirikiane nao katika kuwabaini na kuwaibua wote wanaofanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye maeneo yetu…lakini bila kusahau kuwasaidia wahanga wa ukatili ili wapate haki stahiki,” anasema Mpogolo kwa kumalizia.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa