Leo tarehe 03 Januari, 2025, Wakuu wa Divisheni na Vitengo pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi wameungana na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii, zikiwemo zoezi la upandaji miti na kuwatembelea wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Ikungi.

Shughuli hizo zimefanyika ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya miaka 49 ya Chama cha Mapinduzi (CCM), yakilenga kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuchochea uwajibikaji kwa jamii.

Katika tukio hilo, Umoja wa Wanawake Tanzania pia ulitoa msaada wa taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ikungi, ikiwa ni jitihada za kuwasaidia wasichana kuendelea na masomo yao bila vikwazo vinavyotokana na ukosefu wa mahitaji ya msingi.

Aidha, UWT ilitoa msaada wa mahitaji maalum yakiwemo madaftari, kalamu na sabuni kwa watoto wenye mahitaji maalum wanaosoma katika Shule ya Msingi Mchanganyiko Ikungi, ikiwa ni sehemu ya kuonesha upendo na mshikamano kwa makundi maalum katika jamii.
Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika utekelezaji wa shughuli za kijamii zenye lengo la kuboresha ustawi wa wananchi na kuimarisha

Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania
Simu ya mezani: +255262964037/6
Mobile:
Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz
Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa