• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Waziri Jaffo apongeza mchakato was uchaguzi Singida

Posted on: November 6th, 2019




WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Seleman Jaffo amewapongeza wakazi wa mkoa wa Singida kwa kuwa miongoni mwa mikoa mitano nchini iliyoonyesha hamasa na kujitokeza kwa wingi kitakwimu katika mchakato mzima wa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura, ikiwa ni moja ya hatua muhimu kwenye mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa unaoendelea.

Jaffo aliyasema hayo Novemba 6, 2019 akiwa mkoani hapa, alipotembelea kukagua utekelezaji wa kanuni na taratibu za mchakato wa uchaguzi huo unavyoendelea hatua kwa hatua.

“Katika zoezi la uandikishaji Singida ni miongoni mwa mikoa mitano iliyofanya vizuri sana, na kwa wagombea tayari kwa mfululizo wa siku saba tumekamilisha zoezi la kuchukua na kurudisha fomu na hatimaye kufanya teuzi kwa wenyeviti na wajumbe wa kamati za rufaa,” alisema

Alisema, hali halisi iliyopo mpaka jana ni kwamba jumla ya kata 3956 zilizopo nchi nzima, kimantiki zoezi zima linakwenda vizuri, ingawa kuna baadhi ya maeneo machache zimejitokeza changamoto ikiwemo baadhi ya maeneo wagombea hawakupata fomu kwa wakati.

Aliyataja baadhi ya maeneo hayo kuwa ni Songwe (Vwawa), Arusha (Arumeru), Mwanza na Kilimanjaro (Moshi), huku akizitaka kamati zote za rufaa nchi nzima kuhakikisha wakati wa maamuzi wanasimamia haki na usawa, kwa mujibu kanuni, taratibu na miongozo iliyopo bila ya kumuonea mtu yeyote.

“Azma yetu sote ni kuona uchaguzi huu unakwenda vizuri na unakamilika vizuri…kwa lengo mahususi la kuunda mamlaka za Serikali za mitaa ambazo zinakwenda kujibu matatizo makubwa ya wananchi,” alisema

Aidha, Jaffo alibainisha umuhimu wa zoezi linaloendelea kwa sasa kuwa, uchaguzi huo unakwenda kutengeneza Serikali za mitaa zilizo karibu zaidi na wananchi, ambazo taifa likitoka na ajenda zozote zile za maendeleo basi utekelezaji na msingi wa maendeleo utatoka chini.

Alisema, ifahamike kwa wananchi wote kuwa, kwa mujibu wa kanuni zilizopo, ‘Kamati ya Rufaa ya Wilaya’ inaundwa na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) ambaye ndiye mwenyekiti, akisaidiwa na wajumbe ambao ni watumishi 4 wa sekta za umma kutoka wilaya zote ndani ya mkoa, huku Katibu wa kamati naye atatoka ndani ya sekta ya umma lakini yeye tofauti na wenzake, ataruhusiwa kupiga kura.

“Mwenyekiti nendeni mkazingatie haki, sikilizeni rufaa na malalamiko yote yatakayoletwa mezani kutoka vyama vyote, na watu wote kwa uhuru na upana wake bila kuingiliwa na mtu yeyote,” alisisitiza Jaffo mbele ya wajumbe wa kamati ya rufaa mkoani hapa, na kuongeza;

“Mmepewa rungu lisilokuwa na mashaka…tendeni haki msiogope hakikisheni kila kitu kinanyooka, kama kuna mtu anastahili haki mpeni haki yake na kama kuna kasoro zozote rekebisheni.”

Zaidi, alilitaka Jeshi la Polisi kupitia Makamanda wa mikoa kuendelea kusimamia utaratibu uliowekwa kwa misingi ya Amani, na kamwe mtu yeyote asijitokeze kuchafua mchakato wa uchaguzi unaoendelea kwa maslahi yake binafsi.

Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa ya wilaya ya Singida DC mkoani hapa, Wilson Shimo, alisema kwamba wamejipanga vizuri kusikiliza malalamiko na rufaa zote kwa haki na kurekebisha kwa mujibu wa kanuni zinazowaongoza, huku akiweka wazi kuwa mpaka jana bado walikuwa hawajapokea malalamiko yoyote.

Aidha, Mjumbe mwingine wa kamati hiyo, Patrick Zamba, alisema watajitahidi kutoa maamuzi sahihi kwa muda mwafaka kwa mujibu wa sheria na kanuni, kulingana na kutoridhishwa kwao na maamuzi ambayo yamefanyika.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi, alisema siku zote ‘siku njema daima huonekana asubuhi’ na kwamba hatua ya mkoa huo kupokea hati ya ushindi na kuwa miongoni mwa mikoa 5 bora ni ishara njema.

“Singida ni njema…tena ni njema….na ni njema sana!…na asubuhi hii njema ndio itabeba mchana wote kuwa mwema zaidi, kwa hatua zote mpaka kukamilika kwa mchakato mzima wa uchaguzi huu muhimu,” alisema



MATUKIO KATIKA PICHA

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mhe Seleman Jaffo, akisisitiza jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Rufaa ya Wilaya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Singida wakati alipotembelea kukagua utekelezaji wa kanuni na taratibu za mchakato wa uchaguzi unavyoendelea hatua kwa hatua hapa nchini.

Mkutano ukiendelea.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mhe Seleman Jaffo, akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Rufaa ya Wilaya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Singida wakati alipotembelea kukagua utekelezaji wa kanuni na taratibu za mchakato wa uchaguzi unavyoendelea hatua kwa hatua hapa nchini.


Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi akisikiliza kwa makini hotuba ya Waziri wa OR-TAMISEMI, Seleman Jaffo, wakati wa mkutano huo.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, Sweetbert Njewike akisikiliza kwa makini hotuba ya Waziri wa OR-TAMISEMI, Seleman Jaffo, wakati wa mkutano huo.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza wakati wa mkutano huo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mhe Seleman Jaffo, akipokea shukrani za Serikali ya mkoa wa Singida kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Singida DKt. Rehema Nchimbi (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akifurahia jambo wakati wa mkutano huo.


Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa