• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

HALMASHAURI WILAYA IKUNGI YAPEWA KONGOLE KUPATA HATI SAFI MFULULIZO MIAKA 10

Posted on: June 25th, 2024

HALMASHAURI WILAYA IKUNGI YAPEWA KONGOLE KUPATA HATI SAFI MFULULIZO MIAKA 10

HALMASHAURI ya Wilaya Ikungi mkoani Singida imeng'ara ambapo katika kipindi cha mfululizo wa miaka 10 imepata hati safi kuanzia 2013/2014 hadi 2022/2023.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya, Justine Kijazi, amesema hayo leo Juni 25, 2024 wakati wa kikao maalum cha Baraza la Madiwani cha kujadili majibu ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Amesema kulingana na taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya kuishia Juni 2023,Halmashauri ilikuwa na hoja 5,hoja za miaka ya nyuma ni 24 na hoja za mwaka 2022/2023 ni hoja 28.


Kijazi amesema hoja 30 zilifungqa na kubaki na hoja 22 ambazo ziko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji.

"Tunashukru sana ofisi ya Mkaguzi wa ndani ambayo ni jicho la halmashuri kusimamia hoja,sasa tunajiandaa na ukaguzi wa mwaka 2023/2024,tuendelee kuomba ushirikiano ili halmashuri iendelee kupata hati safi,tutaendelea kufanya kazi kwa kufuata sheria,kanuni,taratibu na miongozo ya serikali,"amesema Kijazi.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Halima Dendego, amesema ni jambo kubwa na la kupongezwa na kitia moyo kwa halmashuri kupata hati safi kwa mfululizo wa miaka 10.

Amesema wakaguzi wa ndani ni walimu wazuri sana ambao kama halmashuri inazingatia ushauri wao halmashuri haiwezi kuwa na hoja nyingi za ukaguzi.

"Katika Halmashauri ukiona hoja zinajitokeza ujue kuna mtu amekula bila kunawa, naagiza kila mzalisha hoja iwe ni idara abanwe," amesema Dendego.

Mkuu wa Mkoa ameagiza kuwa kudhibiti hoja mpya zisijitokeze katika mkutano wa kila mwezi wa Kamati ya fedha ajenda mojawapo iwe ni kujadili hoja za CAG kwani haiwezekani mtu anazalisha hoja halafu watu wanasumbuka kukutana na kuzijadili.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mhe. Ally Mwanga amesema halmashuri hiyo kupata hati safi mfululizo kwa miaka 10 ni kutokana na ushirikiano uliopo wa watendaji na madiwani.


Akizungumza kuhusu hoja za CAG, amesema kimsingi hakuna halmashuri inayofurahia kuwa na wingi wa hoja hivyo jukumu la kila mmoja kuhakikisha hawazalishi hoja mpya.


"Hoja zilizopo ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha zinajibiwa na sio kumuachia Mweka Hazina pekee yake," amesema Mwanga.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida,Dk.Fatuma Mganga, amesema kila halmashauri iweka mkakati madhubuti kujibu hoja za CAG ambapo kila halmashauri ziwe zaidi ya tisa.


Dk.Mganga amesema moja ya vigezo vya kupima utendaji wa halmashuri ni uwingi wa hoja hivyo kinachotakiwa ni kuongeza jitihada kuhakikisha hoja zilizopo zinajibiwa na kutozalisha nyingine.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mhe.Thomas Apson amesema halmashuri hiyo inastahili pongezi kwa kupata hati safi mfululizo kwa miaka 10.


Aidha, Apson amesema halmashuri iongeze ubunifu kwa kuwa na vyanzo vipya vya mapato badala ya kila mwaka kuwa na vyanzo vile vile na kutolea mfano majimoto kwamba kinaweza kuwa chanzo kizuri cha mapato.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa