• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Kufuta hoja kunahitaji umakini na kujitolea

Posted on: June 9th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi leo tarehe 09 Juni, 2025 imefanya kikao maalumu cha Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kwa ajili ya kujadili majibu ya hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2024.

Kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2024, halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 40 kati ya hizo hoja za miaka ya nyuma ni 20 na hoja za mwaka wa fedha 2023/2024 ni 20 hadi sasa, halmashauri imefanikiwa kufunga hoja 9 za miaka ya nyuma na hoja 5 za mwaka wa fedha 2023/2024 hivyo kubakiwa na hoja 26 ambazo zipo katika hatua nzuri za utekelezaji.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Fatuma Mganga, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi, Mheshimiwa Rashid M. Rashid, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mheshimiwa Ally J. Mwanga, Waheshimiwa Madiwani; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndugu Kastori Msigala, wakaguzi kutoka Ofisi ya Ukaguzi Mkoa, pamoja na wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri.

Miongoni mwa masuala yaliyowekwa mezani ni pamoja na umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ili kuondoa hoja au kupunguza idadi ya hoja, ili Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi iendelee kupata hati safi kwa miaka mfululizo.

PICHA NA MATUKIO 






Kikao kilisisitiza kuwa hoja zinazoweza kufutwa ndani ya uwezo wa halmashauri ziondolewe mara moja, huku hoja zinazohitaji fedha zipewe kipaumbele katika vyanzo vya mapato ama ziwekwe kwenye bajeti ili kuweza kupunguza mzigo huo.

Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Ally J. Mwanga, amesisitiza kuwa hoja ni kipimo cha utendaji wa halmashauri

 “Wingi wa hoja si sifa, tunapaswa kuziondoa hoja zilizo ndani ya uwezo wetu na kwa zile zilizo nje ya uwezo, tujibidiishe kwa kila hali kuhakikisha tunazipunguza au kuziondoa kabisa ili halmashauri yetu iendelee kupata hati safi kila mwaka.”

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Fatuma Mganga, aliweka msisitizo kwa Halmashauri kuchukua hatua za haraka kufuta hoja hizo.

Kwa hoja ambazo ni za miaka ya nyuma na zinazohitaji fedha nyingi kufutika, Katibu Tawala alisisitiza kwamba Halmashauri iweke bajeti mahsusi kwa ajili ya kulipa madeni hayo.

“Kufuta hoja kunahitaji umakini na kujitolea, Mkurugenzi hakikisha hoja zinafutika,” alisisitiza.

Kwa kumalizia, Mheshimiwa Mganga aliwataka viongozi na watendaji kufanya kazi kwa ushirikiano (team work) ili kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato.

 “Kila mwaka mapato yanaongezeka, Nampongeza Mkurugenzi Msigala kwa kunihakikishia kuwa mwaka huu halmashauri itakusanya hadi shilingi bilioni 7,  halmashauri isisahau kutenga asilimia 10 ya mapato hayo kwa ajili ya vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.  kama mkataba wa Serikali unavyoelekeza. ” alisema.

Aidha, amehimiza kuwa majibu ya hoja yanapotolewa, yasiwe ya jumla jumla na yenye ushahidi ili kuweza kuwashawishi wakaguzi kufuta hoja husika.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa