• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Utaratibu wa Magari ya Abiria Yafate Utaratibu Uliowekwa Makiungu

Posted on: January 31st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Thomas Apson amesisitiza wamiliki wa magari ya abiria katika kijiji cha Makiungu kufuata  utaratibu wa kupakia abiria Hospitali ya Makiungu na Stendi ya Makiungu kama alivyouweka wakati wa kusuluhisha mgogoro wa stendi mwaka Jana.Katika kikao kilichofanyika hii leo Tarehe 31, Januari, 2024, Mtendaji wa Kata ya  Makiungu Bi-Nasra Abbas Mattaka amesema kuwa uongozi wa wamiliki wa magari, uongozi wa kijiji pamoja na uogozi wa kampuni ya mabasi ya Hope Express walikaa kujadili utaratibu ambao ulikuwa ukikiukwa na kampuni hiyo ambayo imekua ikipakia abiria kinyume na utaratibu uliowekwa hali ambayo inazua mgogoro baina ya wamiliki wa magari mengine."Hali hiyo imepelekea kuleta taharuki kwani tayari utaratibu ulishawekwa baada ya Mkuu wa Wilaya kufanya vikao kadhaa kati ya Uongozi wa Hospitali ya Makiungu na wamiliki wa vyombo vya abiria" Amesema Mtendaji wa kata hiyo.Kwa upande wake mmiliki wa magari ya Hope Express, Bwana Saidi  amesema kinachofanya wakiuke utaratibu uliowekwa na Mkuu wa Wilaya kwa sababu ya ratiba walizopewa na LATRA hali inayowalazimu kupakia abiria mapema ili waondoke kwa muda kuelekea Igunga."Hivyo tunaomba kupakia abiria katika Hospitali ya Makiungu kwa muda wa saa moja kuanzia saa 7 hadi saa 8 kwani hospitali ndipo wanapopatikana abiria wengi zaidi ya stendi", amezungumza Bwana Saidi.Baadhi ya madereva na wamiliki wa magari wamesema hawana tatizo na kampuni hiyo mpya inayofanya safari zake kutoka Igunga mpaka Makiungu. Madereva wamesema cha msingi  Hope Express wafate utaratibu ambao wameukuta kwani ni utaratibu ambao hauleti migogoro  kama ilivyo sasa.Mwisho, Mkuu wa Wilaya amemaliza na kusema kuwa utaratibu aliouweka kwa makubaliano ya pande zote ufuatwe kama ulivyo kwani ndio njia pekee yakuepukana na migogoro."Cha msingi, uongozi wa kampuni ya Hope Express ukae na uongozi wa magari ya abiria kata ya Makiungu ili wapewe zamu na kufuata utaratibu na sio kila gari mpya inayokuja ifuate utaratibu wake wenyewe", amesema Mkuu wa Wilaya ya Ikungi.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Msigala Aagiza kutungwa kwa Sheria Ndogo Kudhibiti chumvi

    May 09, 2025
  • Ikungi Kinara wa Miradi Bora

    May 08, 2025
  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa