• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Yakabidhi Hundi ya Zaidi ya Milioni 278.2 kwa Vikundi 17 Mkopo wa Asilimia 10

Posted on: December 20th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi yakabidhi hundi ya zaidi ya milioni 278.2 kwa vikundi 17 mkopo wa asilimia 10 wa wanawake,vijana na walemavu, hatua Kali kuchukuliwa kwa watakaoenda kinyume na makubaliano yaliyowekwa dhidi ya mkopo huo.

Hayo yamesemwa hii leo tarehe 20 Disemba 2024 katika ukumbi wa Halmashauri na Mhe Ally Mwanga akimuwakilisha Mbunge wa jimbo la Singida mangharibi Mhe Elibariki Kingu kuwa kumeibuka tabia ya vikundi kubadili matumizi ya fedha za mikopo na wengine kukimbia na fedha hizo.

"Hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaofanya hivyo" amesema Mwanga.

Mkurugenzi Mtendaji Ndg Justice Kijazi akisoma taarifa amesema kuwa halmashauri ya wilaya ya Ikungi tayari ilikuwa imeshatoa mikopo yenye thamani ya milioni 852.1kwa vikundi 271 vya wanake vijana na watu wenye ulemavu ambapo kati ya fedha hizo vikundi 186 vya wanawake vilipatiwa mikopo yenye thamani ya milioni  476.9, vikundi vya vijana 58 mikopo ya Shilingi 303.2 na vikundi vya watu wenye ulemavu 27 mikopo ya milioni 71.9 na kupekekea jumla ya wanufaika 1870 walipata mikopo hiyo iliyowawezesha kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi, ufugaji , kilimo biashara ndogondogo na Tehama.

Kijazi ametaja changamoto zilizopo katika utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kuwa ni pamoja na baadhi ya vikundi kutorejesha mikopo kwa wakati, vikundi kubadili matumizi ya fedha walizokopeshwa hata kabla ya kutekeleza miradi waliyoombea fedha, mabadiliko ya hali ya hewa kuathiri miradi ya Kilimo,uhaba na bei kubwa kwa baadhi ya malighafi za miradi hivyo kukwamisha uendelevu wa miradi

Kukosekana kwa mtandao wa usajili kwenye baadhi ya maeneo,uhaba wa vitendea kazi kwa wataalam wanaoratibu mikopo hii hususan usafiri, vifaa vya kusajilia vikundi kwa njia ya kielektroniki laptop na vishkwambi na vifaa vya hamasa kama vile vipaza sauti na kutokuwepo kwa mafunzo ya kina kwa vikundi.

"Kwa niaba ya wananchi wa Ikungi naishukuru Serikali ya Awamu ya 6 chini ya Mhe.Rais Daktari Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa mikopo hii kwa wananchi na kuridhia ianze kutolewa tena baada ya kuboreshwa taratibu wa utoaji na usimamizi wa mikopo hii" amesema Kijazi

Kwa upande wao baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo wameishukuru serikali kwa kushirikiana vyema na Halmashauri ya wilaya ya Ikungi kurejesha mikopo hiyo kwani imekuwa msaada kuinuka kiuchumi hususani wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalimu.

Halmashauri kwa kuzingatia kifungu 8(1) cha Kanuni za utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu za mwaka 2024 ilitangaza kufunguliwa kwa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu na uwepo wa fedha kiasi cha Shilingi milioni 595 kwa uwiano wa 4:4:0

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa