• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Ikungi Singida Sports Promosion Yaanzishwa Ikungi

Posted on: January 30th, 2025

JUMUIYA ya watu wanaoishi nje ya wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida wamesajili taasisi ya kuibua na kuendeleza vipaji vya michezo kwa vijana kwa ajira endelevu ijulikanayo kwa jina la Ikungi Singida Sports Promosion (ISSP) itakayohakikisha michezo katika Halmashauri ya wilaya ya Ikungi inanyanyuka sambamba na vijana kupata ajira kupitia michezo hiyo.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Ikungi Singida Sports Promosion ,Salvatory Alute aliyasema hayo kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi wakati wa hafla ya kuitambulisha taasisi hiyo wilayani Ikungi na kukabidhi msaada wa mipira kwa baadhi ya shule za msingi na sekondari zilizopo katika Halmashauri hiyo.

Mwenyekiti huyo hata hivyo alifafanua kwamba lengo la kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni kuhakikisha kwamba michezo katika Halmashauri hiyo,katika Mkoa wa Singida na baadaye katika nchi nzima inanyanyuka na watoto wanapata ajira,watoto wanarudisha nyumbani kile wanachokipata,uchumi unakuwa katika eneo hilo huku wazazi na jamii kwa ujumla inafaidika.

Aidha Mwenyekiti Alute aliweka bayana kuwa kwa hivi sasa wamebaini kwamba kuna baadhi ya watoto wenye vipaji vya michezo lakini wanaishia kwenye ngazi za chini hawaonekani na hawaonekani kwa sababu hakuna mtu wa kuwasaidia.

“Lakini nishukuru pia kwamba mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi ametupokea vizuri na ameahidi kushirikiana na sisi kwa sababu taasisi kama taasisi haiwezi kuanzisha kitu kipya ila tutaingia katika mifumo ya kiserikali iliyopo kwa mfano mashuleni tutakuwa na kalenda ya shule tutakuwa tunasaidia pale ambapo kalenda ya michezo itakavyokuwa inaonyesha”aliweka bayana mwenyekiti huyo.

Kwa mujibu wa Alute ambaye pia ni Afisa elimu msingi katika Halmashauri ya wilaya ya Arusha kwa sasa hivi wanakwenda kwenye michezo ya Umisseta na Umitashimta kwa hiyo wao kama taasisi watajikita katika kuhakikisha kwamba michezo hiyo inakwenda vizuri kuanzia ngazi ya maandalizi na ushiriki wa watoto unakuwa mpana zaidi.

Kwa upande wake Afisa elimu msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi,Marhareth Kennan Kapolesya alisema kwamba kwa uwezo wake Mungu Halmashauri hiyo ina watu wenye vipaji sana vya kukimbia kwani vitu kama hivyo siyo kama vinapatikana kwenye kila sehemu ,bali hiyo ni zawadi kutoka kwake kwani mungu hutoa zawadi tofauti tofaui kwa kila sehemu.

Akitoa mfano ofisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia sekta ya elimu alibainisha kuwa kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo kwa ngazi ya Mkoa kwenye Umitashimuta Halmashauri hiyo kimkoa imechukua ushindi wa ujumla kwa nyanja zote wapo sawa,lakini kwa kombe la riadha hilo hawana shaka ya wao kulinyakua kwakila mwaka.

Mkuu wa shule msaidizi shule ya sekondari Unyahati,Jofrey Daudi Mianga alijigamba kwamba mwaka uliopita kuna vijana kutoka katika shule hiyo walishiriki michezo ya mbio za marathoni na baadhi yao walienda kushiriki mpaka ngazi ya taifa na kushika nafasi ya pili na kuongeza

kuwa kutokana na uwepo wa taasisi hiyo wanaweza kuhamasika zaidi na kuongeza jitihada kwenye sekta ya michezo.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Msigala Aagiza kutungwa kwa Sheria Ndogo Kudhibiti chumvi

    May 09, 2025
  • Ikungi Kinara wa Miradi Bora

    May 08, 2025
  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa