• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Ikungi Yaibuka kidedea Mbio za Mwenge 2024

Posted on: October 16th, 2024

WILAYA  ya Ikungi mkoani  Singida wamekuwa washindi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 kwa Kanda ya Tatu, na kuweza kukabidhiwa kikombe na fedha sh. milioni moja, huku wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Halima Dendego.Ikungi imeshinda kwenye Kanda ya Tatu yenye mikoa ya Ruvuma, Singida, Dodoma, Manyara, Kagera na Mara, ikiwa ni ishara kuwa walikidhi vigezo kuanzia mapokezi ya Mwenge wa Uhuru, hamasa, na ubora wa miradi ikiwemo miradi kuakisi thamani ya fedha, na kuwepo kwa vielelezo vyote vya manunuzi na vifaa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Oktoba 15, 2024,  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Justice Kijazi, alisema ushindi huo ni wa wananchi wa Wilaya ya Ikungi na mkoa wote wa Singida, na imewapata moyo kuweza kuendelea kufanya  vizuri katika utekelezaji wa miradi.Kijazi amesema wao kama viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia shughuli za maendeleo ikiwemo miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu, fedha za mapato ya ndani ya halmashauri, wananchi na wafadhili, watahakikisha inakamilika na kuwanufaisha wananchi.Kijazi amesema Mwenge wa Uhuru 2024 katika Wilaya ya Ikungi umezindua, kuweka mawe ya msingi na kutembelea miradi saba yenye thamani ya sh. 3,046,807,381. Na miradi hiyo ipo kwenye sekta ya elimu, maji, afya, mazingira, barabara, ujenzi na maendeleo ya jamii.

 "Chanzo cha fedha za miradi hiyo, Serikali Kuu sh.2,889,821,381, wananchi sh. milioni 120, wahisani sh  24,486,000, na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi sh. milioni 12.5" amesema Kijazi. Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Godfrey Mnzava amesema moja ya changamoto kwenye halmashauri hapa nchini ni kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi kwa kutumia fedha za mapato ya ndani. Lakini pia, miradi inayotekelezwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kushindwa kukidhi haja ya wananchi, hivyo kwenye Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, maeneo hayo mawili yapewe kipaumbele kwenye kuangaliwa.CHANZO NIDm new Online

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Mafunzo ya BVR Awamu ya Pili yazinduliwa

    May 14, 2025
  • Msigala Aagiza kutungwa kwa Sheria Ndogo Kudhibiti chumvi

    May 09, 2025
  • Ikungi Kinara wa Miradi Bora

    May 08, 2025
  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa