Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Binilith Mahenge alipokuwa akizungumza katika mkutano maalumu wa baraza la waheshimiwa madiwani lililofanyika tarehe 9 june 2021, wakati wa kujadili majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia juni 30, 2020.
Akitoa pongezi hizo alimshukuru mwenyekiti wa Halmashauri kwa kumkaribisha kwenye kikao hicho, Pia alitoa pongezi kwa halmashauri ya wilaya ya Ikungi kwa kufanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mapato. Alisisitiza kila idara iwajibike na kusimamia mapato ya halmashauri na sio kuachia idara moja.
HABARI PICHa
Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania
Simu ya mezani: +255262964037/6
Mobile:
Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz
Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa