• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya Mifugo Yazinduliwa Rasmi

Posted on: July 8th, 2025

Katibu Tawala Wilaya ya Ikungi Mhe.Rashid M.Rashid akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Thomas Apson amezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya chanjo ya mifugo katika kijiji cha Mungaa kilichopo jimbo la Ikungi mashariki leo tarehe 08Julai, 2025.


Akizungumza na wananchi wa Mungaa amesama kuwa Kampeni hii ni sehemu ya mpango wa miaka mitano wa Serikali ya awamu ya Sita unaolenga kudhibiti magonjwa ya mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo nchini.


Kampeni hii imeanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na inafadhiliwa kwa ruzuku ya serikali yenye thamani ya Shilingi bilioni 216, ambapo mifugo inachanjwa kwa gharama nafuu ili kufikia soko la kimataifa, lengo kuu ni kuhakikisha angalau asilimia 70 ya mifugo nchini inapata chanjo


DAS ameeleza kuwa Wilaya ya Ikungi ina zaidi ya ng’ombe 418,000, mbuzi 222,000, kondoo 79,000 na kuku zaidi ya 900,000 hivyo wilaya imepokea chanjo zaidi ya milioni moja kwa ajili ya kuku, ng’ombe, mbuzi na kondoo, pamoja na hereni za kielektroniki kwa ajili ya utambuzi wa mifugo kwa huyo.


"Nawasisitiza wafugaji wote muwe mstari wa mbele kuwapa mifugo yenu chanjo hizi ili kuweza kupata mifugo inayokizi soko la kimataifa" amezungumza DAS


Mheshimiwa Rashid ametaja bei elekezi ya chanjo ya homa ya mapafu kwa ng’ombe inatolewa kwa Shilingi 500, kwa mbuzi na kondoo ni Shilingi 300, huku chanjo kwa kuku ikiwa bure, aidha viongozi wa vijiji na vyama vya wafugaji wametakiwa kushirikiana kuhakikisha wafugaji wanapeleka mifugo yao katika vituo vya chanjo.


Mwisho ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kuchanja mifugo yao, na kufuata hatua nyingine za kinga kama kuogesha mifugo, kutoa tiba sahihi na kufuata karantini pale mlipuko unapotokea.


Kwa upande wake Afisa Kilimo Wilaya ya Ikungi Ndg. Issa Mtweve amesema anaishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuleta mpango wa chanjo ya rukuzu na kuwataka wafugaji kutumia fursa hiyo kwa kujitokeza kuchanja mifugo yao.


"Kampeni hiyo itaendelea katika vijiji vyote vya wilaya ya Ikungi kuhakikisha elimu inatolewa na mifugo yote inapata chanjo kwa muda elekezi" ameongeza Mtweve

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Ziara ya Ukaguzi wa Miradi Siku 10 Kabla ya Mwenge, RC Dendego Apongeza

    July 12, 2025
  • Ripoti ya Utafiti wa Msitu wa Minyughe Yatolewa, Matarajio Mema Ikungi

    July 10, 2025
  • Elimu Itolewe Mfumo wa Stakabadhi Ghalani

    July 09, 2025
  • Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya Mifugo Yazinduliwa Rasmi

    July 08, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa