Kwa mujibu wa Hotuba ya Mwenyekiti wa kamati ya Usalama Wilaya ya Ikungi Mhe Thomas Apson Tarehe 30 Novemba 2023 katika Kongamano la kujadili na kupinga ukatili katika jamii alisema kuna viashiria vingi vya ukatili wa kijinsia wilayani hapa hali inayopelekea watu Kujinyonga,Ndoa kuvunjika,Kuongezeka kwa migogoro kwenye jamii na wengine kushindwa kuendelea na masomo yao kutokana na ukatili mbalimbali wanaofanyiwa.Katika Kongamano hilo washiriki waliazimia mambo mbalimbali yatakayosaidia kumaliza swala la ukatili Wilaya ya Ikungi na nchini kwa ujumla ikiwa ni pamoja na Kutolewa kwa Elimu ngazi zote,Jamii itoe taarifa za ukatili ili serikali Kuchukua hatua za kisheria kwa wanaosababisha ukatili,Kufanyika kwa makongamano ya mara kwa mara kujadili hali ya ukatili katika jamii,Serikali kutenga maeneo ya biashara kwa walemavu ili kuepukana na maswala ya Ukatili na Mengineyo."Hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa juu ya changamoto hiyo, kubwa ikiwa ni pamoja na elimu kutolewa ngazi zote kuanzia Wilaya mpaka ngazi za vijiji na vitongoji ili kupunguza ukatuli kama sio kumaliza kabisa tatizo hilo" Alisema Mkuu wa Wilaya ya IkungiTarehe 21 Agosti 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ilipokea mradi wa pamoja wa kuongeza kasi ya uwezeshaji wa Wanawake wa kijijini kiuchumi unaotekelezwa katika kata tano ikiwa ni pamoja na Kata ya Ikungi,kata ya Dung'unyi na kata ya Puma,Kata ya Irisya na Sepuka unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya WFP,IFAD,FAO na UNwomen kwa ufadhili wa serikali ya Norway na SweedenAfisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe amesema kuwa kwa Tanzania mradi huu unatekelezwa Wilaya tatu pekee ikiwa ni pamoja na Wilaya ya Ikungi.Nnamo Tarehe 24 Agosti 2023 Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndg Justice Kijazi Alifungua mafunzo ya mradi huo Wilayani Ikungi yaliyotolewa na Kampuni ya KIVULINI na kusema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wanamabadikiko kwani yatasaidia mradi huo kufanyika kwa ufanisi na juhudi kubwa lengo kuu ikiwa ni pamoja na kubadili fikra za jamii nzima kuwa na mtazamo chaya.Afisa maendeleo aliongeza na kusema lengo lingine pia ni kutokomeza mimba za utotoni,Ndoa za utotoni.
Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania
Simu ya mezani: +255262964037/6
Mobile:
Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz
Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa