• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Maandamano ya Amani ya Kumpongeza Mh.. Rais Magufuli kwa kurejesha kikokotoo cha zamani

Posted on: January 5th, 2019


Baada ya Rais Dkt. John Magufuli kurejesha Kikokotoo cha zamani kwa mafao ya WATUMISHI WA UMMA nchini, wafanyakazi kupitia mashirikisho huru ya vyama  wameendelea kuunga mkono agizo hilo kwa kufanya  maandamano ya amani.

Shirikisho huru la vyama vya wafanyakazi Mkoa wa Singida, leo limefanya maandamano ya amani ya kumpongeza Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kwa kuondoa tatizo la KIKOKOTOO ambacho kilisababisha watumishi wengi kukosa amani na utulivu mioyoni mwao.

Maandamano hayo yaliyoanzia ofisi za TUCTA mkoa zilizopo mtaa wa Mughanga na kupitia mtaa wa Boma road kisha kupokelewa katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida na Dkt. Rehema Nchimbi ambaye ndiye mkuu wa mkoa wa Singida akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa Vyama na Serikali.


Katika risala ya watumishi hao iliyosomwa na Katibu wa TUCTA mkoa, Bw. Max Chaba, wafanyakazi hao wamepongeza hatua ya Mheshimiwa Rais Magufuli kurejesha kikokotoo cha zamani, hali waliyoieleza kuwa amesikiliza maombi yao na sasa amefuta machozi yaliyokuwa yakiwatoka kwa muda mrefu sana.

Katibu huyo wa TUCTA amesema kuwa, uamuzi wa Rais Magufuli umepokelewa kwa furaha sana na watumishi wote wa mkoa wa Singida na Tanzania kwa ujumla.

“Uamuzi huu umerejesha hali na morali ya watumishi wa umma nchini katika kufanya kazi kwa nguvu zao zote. Hii inatokana na imani kwamba baada ya kustaafu kuna kitu ambacho watakipata chenye nafuu cha kumwezesha kujikimu yeye mwenyewe na familia yake” Bw. Max amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TUCTA mkoa wa Singida, Bw. Emmanuel Misholi, amesema kikokotoo kilichotangazwa awali kilikuwa ni JENEZA lililoandaliwa kwa ajili ya watumishi wanaotarajiwa kustaafu.


“Kwa kweli Rais Magufuli ni kiongozi msikivu mno amesikia kilio chetu na kuchukua hatua stahiki. Binafsi nina furaha na amani moyoni haijawahi kutokea. Sisi kama watumishi wa umma, hatuna zawadi ya kumpa Dkt. Magufuli isipokuwa ni kuchapa kazi na kukidhi mahitaji ya Watanzania wote bila ubaguzi” amesema Misholi.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amempongeza Rais kwa uamuzi wa busara, huku akiwataka watumishi wa mkoa wa Singida kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Magufuli kwa kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kuleta ufanisi.


Mkuu huyo wa mkoa wa Singida, amewataka watumishi wa umma mkoani hapa kutumia furaha yao na amani waliyoipata baada ya kikokotoo kufutwa, kuongeza  bidii ya kazi mara dufu katika kuitumikia Serikali na Watanzania ikiwa ni kumshukuru Rais Magufuli kwa kusikia kilio chao hicho cha muda mrefu.

Aidha, Dkt. Nchimbi amewaagiza wakuu wote wa idara, vitengo na viongozi wengine mkoani Singida, waendelea kuwa karibu na watumishi walio chini yao, na tabia ya kukemea, kuwatishia, isiwepo ili kumfanya mfanyakazi kuwa na amani wakati wote awapo kazini.

“Wafanyakazi, jambo hili ambalo mmelitambua na kuja kulisherekea leo kwa maandamano ya amani kwa ajili ya kumpongeza na kulitolea shukrani kwa Mheshimiwa Rais Magufuli ni jambo kubwa sana kwa uhai na uhai endelevu wa utumishi wetu na matunda ya kazi zetu”

“Hakika hakukukuwa na namna nyingine yoyote ya kusema isipokuwa ni kutoka na kusema hongera mheshimiwa Rais asante sana kwa haya yote uliyotufanyia na hasa la kutuondolea tatizo hili la kikokotoo… hongera mheshimiwa Rais Magufuli”.


“Waheshimiwa sana wafanyakazi, mnahaki tena mnahaki sana ya kumpongeza Rais na hata mngeamua kushinda kutwa nzima hapa kwa kumpongeza Rais mnahaki, na msiishie hapa endeleeni kumpongeza popote pale, hata mkiwa kwenye madawati yenu endeleeni kumpongeza. Hili la kikokotoo hili, sio letu ni la familia zetu na taifa kwa ujumla” amesema Dkt. Nchimbi kwa furaha tele.


Awali akizungumza baada ya kupokelewa maandamano, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Bw. Juma Kilimba, aliwaomba watumishi wa umma kufanya kazi karibu zaidi na Serikali yao ili kuunga mkono utekelezaji wa sera za Chama Cha Mapinduzi.

  

Kanuni ya kikokotoo kipya kilichokuwa kinalipa asilimia 25 ya mafao ya watumishi, kililalamikiwa sana na kupingwa na wadau wengi nchini, hali iliyomlazimu Rais Magufuli kuingilia kati na kurejesha utaratibu wa zamani.

Maandamano haya yameaandaliwa na chama cha wafanyakazi TUCTA mkoa wa Singida kwa ushirikiano na vyama vya CWT, TUICO, TALGWU, TUGHE, RAAWU pamoja na TAMICO kwa lengo la kumshukuru na kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kufuta kikokotoo.

"Mheshimiwa Rais John Magufuli Oyeeee"!!!

Oyeeeeeeeee!!!" Ndivyo sauti za shangwe na vifijo vilivyokuwa vikitawala kwenye sherehe hizi za pongezi kwa Rais kutoka kwa waandamanaji hao.


MATUKIO KATIKA PICHA 



















Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa