• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Mafunzo ya BVR Awamu ya Pili yazinduliwa

Posted on: May 14th, 2025


Mafunzo kwa waandishi wasaidizi na waendesha mashine za BVR (Biometric Voter Registration) yamefunguliwa rasmi leo 14, May 2025, katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura – Awamu ya Pili, unaotarajiwa kufanyika tarehe 16 hadi 22 ,Mei 2025.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Afisa Mwandikishaji wa Wilaya ya Ikungi, Dkt. Anthony Mwangolombe, aliwataka washiriki kuyazingatia mafunzo kwa makini ili waweze kutekeleza jukumu hilo la kitaifa kwa weledi, ujuzi na uadilifu wa hali ya juu.

“Ninawasihi mzingatie mafunzo haya kwa umakini. Zoezi hili linahitaji umahiri, nidhamu na uaminifu mkubwa kwa kuwa ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025,” alisema Dkt. Mwangolombe.

Mafunzo hayo yamekwenda sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura, ambapo majina ya wapiga kura yamebandikwa katika vituo walivyojiandikishia, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea uandikishaji rasmi.

Washiriki wa mafunzo hayo wanajumuisha waandishi wasaidizi, waendesha BVR, maafisa wasaidizi waandikishaji wa majimbo na kata, pamoja na wakufunzi kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Zoezi rasmi la uandikishaji wapiga kura wapya na uboreshaji wa taarifa litafanyika kuanzia tarehe 16 hadi 22 Mei, 2025, katika kata zote za majimbo ya Ikungi Mashariki na Ikungi Magharibi. Jumla ya vituo 72 vya uandikishaji vitatumika katika kipindi hicho.

Dkt. Mwangolombe alibainisha kuwa:

“Uboreshaji huo utahusisha kuandikisha wapiga kura wapya ambao ni raia wa Tanzania wenye umri wa miaka 18 na zaidi, au watakaotimiza umri huo kufikia siku ya uchaguzi mkuu mwaka 2025. Pia, wapiga kura waliopoteza au kuharibu kadi zao watapewa kadi mpya, na wale walioandikishwa awali watapewa fursa ya kurekebisha taarifa zao, zikiwemo majina na taarifa nyingine muhimu.”

Aidha, aliongeza kuwa mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya uandikishaji wakati wa uboreshaji wa daftari hilo, ili kusaidia kuimarisha uwazi na kuwasaidia kutambua waombaji wa maeneo husika.

“Tume imetoa vibali kwa jumla ya asasi za kiraia 157 kutoa elimu ya mpiga kura wakati wa uboreshaji wa daftari. Ni muhimu wadau wote kushirikiana na asasi hizo ili kufanikisha zoezi hili,” alisisitiza.

Vilevile, alieleza kuwa taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au majimbo waliyosajiliwa awali zitahamishwa, na taarifa za wale waliopoteza sifa za kuwamo kwenye daftari – kama waliofariki dunia – zitaondolewa.

Mwisho wa hotuba yake, Dkt. Mwangolombe aliwatakia washiriki mafunzo mema na kuhitimisha kwa kusema:

“Ninawatakia mafunzo mema na utekelezaji mzuri wa jukumu hili muhimu lililo mbele yenu. Na sasa, natamka rasmi kuwa mafunzo haya yamefunguliwa.”

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Mafunzo ya BVR Awamu ya Pili yazinduliwa

    May 14, 2025
  • Msigala Aagiza kutungwa kwa Sheria Ndogo Kudhibiti chumvi

    May 09, 2025
  • Ikungi Kinara wa Miradi Bora

    May 08, 2025
  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa