• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA YAZINDULIWA WILAYANI IKUNGI

Posted on: August 4th, 2025

Mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata yamezinduliwa leo tarehe 4 AGOSTI 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Mafunzo hayo ya siku tatu yanawajumuisha washiriki 56 kutoka kata 28 za halmashauri hiyo.

Uzinduzi wa mafunzo hayo umehudhuriwa na viongozi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo na kata, maafisa TEHAMA, Afisa Uchaguzi, Afisa Manunuzi na watendaji mbalimbali wa Tume.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Ikungi, Bi. Edina Palla, aliwapongeza washiriki kwa kuchaguliwa kutekeleza jukumu hilo muhimu. Alisisitiza kuwa wanapaswa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria.

“Dhamana mliyopewa ya kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Madiwani wa Tanzania Bara ni kubwa, nyeti na muhimu kwa mustakabali wa taifa letu,” alisema Bi. Palla.

Aliongeza kuwa ni muhimu kwa wasimamizi hao kuzingatia maadili ya kazi, uwajibikaji na weledi katika kipindi chote cha utumishi wao kwa Tume hadi kukamilika kwa uchaguzi mkuu.


“Vishirikisheni vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote za uchaguzi kwa kuzingatia matakwa ya Katiba, Sheria, Kanuni na Maelekezo ya Tume,” alisisitiza.


Kwa upande wake, Afisa Uchaguzi wa Wilaya ya Ikungi, Mwalimu Andrew Marwa, aliwataka washiriki kuwa makini katika mafunzo hayo na kuhakikisha wanayatumia ipasavyo wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.


“Mzingatie Katiba, Sheria, Miongozo na Maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume ili kuhakikisha zoezi la uchaguzi linafanyika kwa amani na mafanikio,” alisema Marwa.


Mafunzo hayo yanatarajiwa kuwajengea uwezo Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya kata katika kusimamia uchaguzi kwa uadilifu, weledi na kwa kuzingatia taratibu zote za kisheria

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • MAFUNZO YA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA YAZINDULIWA WILAYANI IKUNGI

    August 04, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Awataka Vijana Kujishughulisha

    July 23, 2025
  • Pongezi Mradi wa Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari ya Amali Samamba

    July 23, 2025
  • Ziara ya Ukaguzi wa Miradi Siku 10 Kabla ya Mwenge, RC Dendego Apongeza

    July 12, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa