• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

NEST yarahisisha manunuzi

Posted on: March 4th, 2025

kungi, Machi 4, 2025

Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Ugavi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Bi. Mariam A. Haroun, amemwaga sifa tele kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitambua mchango wake mkubwa katika maendeleo ya nchi.


Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Mariam, ambaye ni mmoja wa viongozi wanawake waliobobea katika sekta ya manunuzi na ugavi, amepongeza juhudi za Rais Samia kwa kuimarisha sekta hiyo na kuongeza uwazi katika mifumo ya ununuzi wa umma.


Mariam amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi, zikiwemo Mratibu wa Nchi katika Shirika la AMCA, linalojihusisha na tafiti mbalimbali, hususan kuhusu magonjwa ya mama na mtoto; Meneja wa Ghala katika Kampuni ya Resolute Mining; Mkaguzi Mkuu katika taasisi ya kifedha Abagamba Kamoi SACCOS; na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Ugavi wilayani Monduli.Kwa mujibu wa Mariam, uongozi wa Rais Samia umeleta mabadiliko chanya, hasa katika sekta ya manunuzi na ugavi kupitia mfumo mpya wa kisasa.


"Tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha Mfumo wa Manunuzi wa Taifa (NEST), ambao umeongeza uwazi na kurahisisha mchakato mzima wa manunuzi. Mfumo huu utasaidia vijana wa kike na wa kiume kujiajiri na kujitegemea kiuchumi," alisema Mariam.


Aidha, aliwahimiza wanawake kujitokeza kwa wingi kushika nafasi za uongozi, akisisitiza kuwa wanawake wana uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii na uchumi wa taifa.


"Tunahitaji kuona wanawake wengi zaidi wakiongoza katika sekta mbalimbali. Hakika tunaweza!" alisisitiza.


Kwa kumalizia, Mariam alimtakia Rais Samia heri na baraka ili aendelee kuongoza taifa kwa mafanikio makubwa zaidi.


"Tunaendelea kumuombea Mheshimiwa Rais, ili aendelee kutuongoza kwa hekima na busara," alisema.


Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi kwa kutambua mchango wa wanawake katika jamii, siasa, na uchumi, pamoja na kuhamasisha usawa wa kijinsia katika sekta zote.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa