• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

RC Dendego Aongoza Ukaguzi wa Miradi ya Mwenge wa Uhuru Wilayani Ikungi

Posted on: May 22nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego ameongoza ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Ikungi, akiwa ameambatana na Katibu Tawala wa Mkoa Dkt. Fatuma Mganga pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Ikungi, ikiwa ni maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.

Katika sekta ya elimu, viongozi hao wametembelea mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Samamba (Utaho 'A') unaogharimu shilingi milioni 544.2 fedha zilizotolewa na Serikali Kuu.


Kwa upande wa maji, ukaguzi umefanyika katika mradi wa maji wa Utaho 'A' unaogharimu shilingi milioni 300 ukitekelezwa kwa ufadhili wa wahisani. Aidha, mradi mwingine wa maji eneo la Wibia umehusishwa pia, wenye thamani ya shilingi milioni 60 ukifadhiliwa na Serikali Kuu.

Katika sekta ya afya, ujenzi wa walkways katika Hospitali ya Wilaya ya Ikungi umeangaliwa kwa makini. Mradi huo wa thamani ya shilingi milioni 195 umetekelezwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu na utatembelewa na Mwenge wa Uhuru.


Miradi ya barabara pia imechukua nafasi muhimu, ambapo barabara inayosimamiwa na TANROADS pamoja na ile mpya ya TARURA zimetembelewa ili kuhakikisha maandalizi yanaendelea kwa kasi na ubora unaotakiwa kabla ya ujio wa Mwenge wa Uhuru.


Kwa upande wa maendeleo ya vijana, viongozi hao wametembelea mradi wa Kikundi cha “Ikungi Boys” ambao umetekelezwa kwa gharama ya milioni shilingi 10 kwa mchango wa Halmashauri.


Katika eneo la utawala, ujenzi wa jengo la ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeangaziwa, mradi unaogharimu shilingi milion 263 ukiwa umefadhiliwa na Serikali Kuu.


Akizungumza baada ya ukaguzi, Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego amesema kuwa miradi hii iendane na mahitaji ya wananchi waliopo katika eneo husika ili iwe na tija na kuleta matokeo chanya katika maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe.Thomas Apson ameshukuru na kusema kuwa ukaguzi wa miradi katika Wilaya ya Ikungi umeonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya mkoa wa Singida katika kusimamia maendeleo ya wananchi kupitia miradi ya afya, elimu, maji, vijana na miundombinu.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa