• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Taarifa ya uwepo wa ugonjwa wa kipindupindi katika kata ya Mgungira, Maagizo yatolewa

Posted on: October 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Thomas Apson apokea taarifa ya uwepo wa ugonjwa wa kipindupindi katika kata ya Mgungira kijiji cha Ufana na kata ya Mwaru kijiji cha Kaugeri pamoja na maeneo yaliyokaribu na bwawa la kuvua samaki Wembere.

Akizungumza katika kikao cha PHC katika ukumbi wa Halmashauri

Mkuu wa Wilaya ameagiza kufungwa kwa bwawa la uvuvi wa samaki la Wembere lililopo maeneo yanayozunguka kata ya Mgungira ili kuepusha kuenea kwa ugonjwa huu katika maeneo mengine kuzunguka eneo hilo.

Hata hivyo timu ya wahudumu wa afya wanaendelea kutoka matibabu kwa watu wenye viashiria vya ugonjwa huo wa kipindupindu na kutoa rai kwa wananchi kutumia maji Safi na salama majumbani, na kunawa maji tiririka na sabuni mara watokapo chooni.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victorina Ludovick, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Katibu Tawala Wilaya ya Ikungi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya pamoja Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ikungi wameungana kujadili mlipuko huo huku wakiunga mkono mawazo ya kitaalamu ya watoa huduma wa afya pamoja na maagizo ya Mkuu wa Wilaya ya kufunga bwawa pamoja na kuchimbwa visima vya maji Safi na salama, ujenzi wa vyoo bora katika maeneo hayo kunusuru adha iyo kwa haraka.

Akisoma taarifa hiyo Afisa Afya Brayson Shoo amesema kuwa Kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyoshambulia mfumo wa chakula na kusababisha kuharisha majimaji yanayofanana na maji ya mchele na huweza kuambatana na kutapika hivyo kupoteza maji mengi mwilini.

Ameongeza na kusema kuwa ugonjwa huu unaambukizwa kwa kula vyakula au kunywa maji yaliyochafuliwa au yenye kinyesi cha binadamu chenye vijidudu au vimelea vinavyoeneza Kipindupindu.


Mwisho wataalamu wa afya wameomba kuongezewa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na mahitaji mengine muhimu katika kambi ya kipindupindu kwa haraka kufanya juhudi za kunusuru hali hiyo Katika kata ya Mgungira na Mwaru Wilayani hapa.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa