• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

Posted on: June 18th, 2025

Watendaji wa vijiji wasioweza kutimiza majukumu yao wametakiwa kuchukuliwa hatua za haraka, kauli hiyo imetolewa jana tarehe 18 June, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ndugu Kastori Msigala, alipokuwa kwenye ziara ya kufuatilia na kukagua miradi ya maendeleo katika Kata ya Iglanson.

Msigala amesema Afisa Utumishi anatakiwa kuwachukulia hatua za haraka watendaji wote wa vijiji ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya kila siku huku wakiendelea kupokea mishahara, amesisitiza kuwa haiwezekani mtendaji wa kijiji kushindwa kusimamia na  kukusanya mapato na kuruhusu biashara kufanyika kiholela, hali hii inafanya  Halmashauri kukosa mapato ya ndani ambayo ni muhimu kwa maendeleo.

Akiwa katika Shule ya Msingi Mnyange, Msigala alionesha kusikitishwa na mtendaji wa kijiji kwa kushindwa kuchukua hatua kuhakikisha fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ya kijiji zinatumika kumalizia ufungaji wa madirisha ya aluminium.

"Mtendaji unatakiwa kuwajibika, huwatendei haki watoto, serikali imetoa fedha kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora na mazingira mazuri ya kusomea, kwa nini mpaka sasa hamjatafuta fundi kufunga madirisha?" alihoji Msigala

Katika ziara hiyo, ametembelea pia mradi wa ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Iglanson yenye thamani ya shilingi milioni 46, pamoja na ujenzi wa matundu nane ya vyoo yenye thamani ya shilingi milioni 14.4, na utengenezaji wa madawati 80 kwa gharama ya shilingi milioni 5.5

Katika ukaguzi huo, Ndugu Kastori amesisitiza kuwa mzabuni asilipwe malipo ya mwisho hadi pale atakapokamilisha marekebisho ya kasoro ndogo zilizopo ili mradi huo uendane na thamani halisi ya fedha iliyotolewa na serikali.

Aidha, amekagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Iglanson kilichojengwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 500, kituo hicho kinahudumia zaidi ya wakazi 20,000 na kimejengwa kwa kutumia mfumo wa Force Account.

Akiwa kituoni hapo, amesisitiza kuboreshwa kwa huduma za afya, ikiwemo kuhakikisha mashine kubwa ya kisasa ya kufulia nguo inaanza kufanya kazi mara moja kwa kurekebisha miundombinu ya jengo la Laundri na mifumo yake ya mabomba.

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa fedha nyingi ili huduma bora za afya ziwafikie wananchi hadi vijijini,hivyo ni wajibu wenu kuhakikisha mnawatendea haki wananchi kwa kuwapatia huduma bora za afya," alisisitiza Msigala.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Wachimbaji Wadogo Watakiwa Kuijua Sheria ya Madini na Kanuni Zake

    June 22, 2025
  • Wajasiriamali Kupata Mikopo Ikungi

    June 20, 2025
  • Watendaji wa Vijiji Wanaoshindwa Kutimiza Wajibu Wao Waonywa

    June 18, 2025
  • Hoja 19 Kufungwa Ifikapo Tarehe 19 Juni Mwaka Huu

    June 17, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa