• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Ikungi District Council
Ikungi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi ya Maadili
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ujenzi
      • Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Tekolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Biashara
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango na Utawala
      • Elimu, Afya na Maji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbailmbali
    • Fomu Malimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Vituo vya habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya picha
  • Takwimu za Wilaya
    • Sensa 2022
      • Matokeo ngazi ya Taifa na Mkoa
      • Matokeo ngazi ya wilaya na kata
      • Matokeo ngazi ya vijiji
      • Kasi ya ongezeko la watu
      • Idadi ya kaya
      • Idadi ya watu kwa umri
      • Matokeo ngazi ya tarafa
    • Takwimu za Elimu
      • Orodha ya Shule kwa kata
      • Idadi ya wanafunzi
        • Msingi
        • Sekondari
    • Nyanja ya Afya
      • Idadi ya vituo vya afya kwa kata
      • Afya nyinginezo
    • Ikungi yetu
    • Takwimu za miradi

Waziri wa Maji Mhe. Makame Mbarawa aahidi upatikanaji wa maji Wilaya ya Ikungi

Posted on: February 13th, 2019


Waziri wa Maji Mhe. Makame Mbarawa ameahidi kutoa fedha kwa ajili ya uchimbaji wa visima ishirini (20) na usambazaji wa maji ya bomba kata ya Ihanja na Iseke katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Ahadi hiyo ameitoa Februari 13, 2019 katika kituo cha Afya Ihanja kilichopo katika kijiji cha Ihanja kata ya Ihanja Wilaya ya Ikungi alipokwenda kutembelea kituo hicho ambacho kimekamilisha ujenzi wa majengo saba ya kutolea huduma mbalimbali za Afya.

Akijibu ombi la Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi Ndugu Justice Laurence Kijazi kuhusu upatikanaji wa maji Wilaya ya Ikungi Waziri Mbarawa amesema visima hivyo Ishirini vitachimbwa katika majimbo yote mawili ya uchaguzi ambapo Jimbo la Mashariki litapata visima kumi (10) na Jimbo la Magharibi pia litapata visima kumi (10).

Katika usambazaji wa maji ya bomba kijiji cha Ihanja na Iseke Waziri Mbarawa amesema kuwa atatoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa pampu na uwekaji wa umeme katika kisima cha Iseke ambapo fedha ziatakazotolewa ni za kununulia transforma na nguzo za umeme ili kufanikisha hilo amemtaka Mhandisi wa maji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi Ndugu Victor Kamote kuandaa makadirio ya ghrama za kazi hiyo na kuziwasilisha kwake haraka sana ili aweze kuzifanyia kazi.

Aidha katika mradi huo pia Mbuge wa Singida Magharibi Mhe. Elibariki Kingu ameahidi kutoa shilingi milioni Ishirini kutoka katika mfuko wa Jimbo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi ndugu Ali Mwanga ameahidi Halmashauri itatoa shilingi milioni arobaini. Fedha hizo zitafanikisha kununulia mabomba ambayo yatatoa maji kutoka kisima kilichopo Iseke hadi maneo ya vijiji hivyo viwili ikiwemo kituo cha Afya Ihanja.

Awali akitoa taarifa ya hali ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Ikungi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndugu Justice Kijazi amesema hali ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi sio ya kuridhisha. Akitoa takwimu za watu wanaopata maji safi na salama Mkurugenzi Kijazi amesema Idadi ya wakazi wanaopata maji safi na salama ni 126,195 ambao ni sawa na asilimia 40.1 tu ya idadi ya watu wote 309,031 (projection 2019 kutokana na sense ya 2012) wa Wilaya ya Ikungi. Ndugu Kijazi ameongezea kusema kuwa wakazi wengi wa Wilaya ya Ikungi wanategemea vyanzo vya maji ambavyo si salama na mara nyingine sio vya uhakika.

Pia amesema baadhi ya wakazi hulazimika kutembea umbali mrefu na kutumia muda mwingi kufuata maji ya kutumia majumbani.

Katika kukabiliana na hali ya ukosefu wa maji Mkurugenzi Mtendaji alimweleza Waziri kwamba mkakati uliopo ni kwa Halmashauri ya Wilaya imepanga kujenga na kukarabati miradi ya maji katika vijiji vya Mtunduru, Ighuka, Isuna, Sambaru, Mnane, Mkunguakihendo, Iseke na Sakaa katika mwaka wa fedha 2018/2019.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo aliongeza kusema pamoja na malengo hayo ya upatikanaji wa mji Halmashauri ya Wilaya inachangamoto zinazokwamisha kutekeleza kwa ufanisi kwa miradi. Changamoto hizo ni pamoja na fedha za miradi ya maji kutofika kwa wakati kutoka Wizarani kama ilivyopangwa. Idara ya maji ya Halmashauri ya Ikungi kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha kama gari kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji utekelezaji  wa miradi, ukosefu wa vifaa vya kufanyia utafiti (survey) vifaa vya kupima ubora wa maji na vifaa kwa ajili ya ukarabati wa pampu na mabomba.

Waziri Makame Mbarawa alifika katika kituo cha Afya cha Ihanja kukagua tatizo la upatikanaji wa maji kituoni hapo akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Singida. Katika ziara hiyo pia alifika kijiji cha Ulyampiti kuona chanzo cha maji ya bomba yanayosambazwa kijijini hapo. Katika msafara wake aliongozana na Mwenyekiti wa bodi ya maji Mkoa wa Singida Ndugu Deocres Kamara na wataalamu mbalimbali wa sekta ya maji na Afya kutoka Mkoa wa Singida.

Matangazo

  • MPYA! MPYA! MPYA! TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPT 06, 2023 August 31, 2023
  • View All

Habari mpya

  • Elimu ya Kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yahitajika Ikungi

    April 17, 2025
  • Kamati ya Siasa Yapongeza Ujenzi wa Miradi Ikungi

    April 09, 2025
  • "Wanaume Hudumieni Wake Zenu" DC Apson Ikungi

    March 04, 2025
  • NEST yarahisisha manunuzi

    March 04, 2025
  • View All

Video

DC Muro atembelea Kata ya Mkiwa na kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya sekondari Mkiwa. Kazi inaendelea...
More Videos

Viunganishi vya haraka

Tovuti unganifu

  • EGA website
  • public service management
  • TAMISEMI website
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi

    Anuani ya Posta: S.L.P 42, Singida, Tanzania

    Simu ya mezani: +255262964037/6

    Mobile:

    Barua pepe: ded.ikungidc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi. Haki zote zimehifadhiwa